The reliable source of sport news

Jumapili, Julai 28, 2013

Jose Mourinho asema Juan Mata ni kifaa cha kazi

28.7.13 By Unknown No comments

Jose Mourinho ameelezea mipango yake kumtumia Juan Mata msimu huu, jambo linaloonekana kumaliza tetesi kwamba nyota huyo angeondoka Chelsea.
Muhispania huyo aliripotiwa kuwa miongoni mwa wachezaji wasiomvutia bosi wa Chelsea Mourinho, pamoja na kutajwa mara kadhaa kwenye tuzo ya mchezaji bora wa klabu wa msimu, lakini Meneja wa Chelsea Jose Mourinho amesisitiza kwamba Mata ana mchango mkubwa Chelsea.
‘Hata hivyo anafaa kwenye plan zangu,’ alisema Mourinho. ‘ Ninajua mahali pa kumtumia, mahali anapopata ugumu ndipo anapofanya vema.
‘Tutajaribu kumsaidia kufanya vizuri zaidi maeneo yanayomshinda. Huwa napenda sana kuwatumia wachezaji wanaochezea mguu wa kulia kucheza kushoto.

‘Nilianza na (Arjen) Robben na (Damien) Duff, kisha (Goran) Pandev nikiwa Inter, na (Angel) Di Maria pamoja na (Mesut) Ozil. Kila klabu hufanya hivyo, ni nzuri.
‘Napenda winga anaposhuka na kupenyeza  kwa ajili ya mashambulizi kwa pasi, na mashuti pia. Juan ni mchezaji pekee tuliye naye atakayefanya hilo upande wa kulia.’
‘Upande wa kushoto tuna (Eden) Hazard, Victor Moses, Kevin De Bruyne, Andre Schurrle. Juan anakuwa huru sana kucheza namba 10 pia. Kati ya sehemu hizi mbili ana mengi ya kuifanyia timu.’


0 comments:

Chapisha Maoni