The reliable source of sport news

Jumatano, Julai 24, 2013

Barcelona imethibitisha kwamba Martino ndiye kocha mteule na kuna uwezekano kuwa atambakisha Fabregas Barca

24.7.13 By Unknown No comments

Barcelona imethibitisha kwamba Mwajentina Gerardo Martino ndiye kocha mteule wa timu hiyo kufuatia kujiuzulu kwa Tito Vilanova kwa sababu za kiafya.

Kutoka kwenye tovuti ya Barca, mabingwa hao wa Hispania wamesema:

"Gerardo Martino, kocha mpya FC

Barcelona. FC Barcelona imefikia makubaliano kumsajili Gerardo Martion kama meneja wa kwanza wa klabu hiyo kwa misimu miwili ijayo."

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 50 ambaye pia ni meneja wa zamani wa Newell's Old boys atakuwa Mwargentina wa nne kushika wadhifa huo katika historia ya klabu ya Catalans kufuatia Roque Olsen, Helenio Herrera na Cesar Luis Menotti.

"Sikuwa nimetarajia hili, Nilikuwa nikijiandaa kupumzika mara nilipopokea simu toka Barca, najivunia kupata fursa hii." Martino aliiambia tovuti ya Barcelona. "Nina furahi sana Barcelona kunifikiria kwa kazi hii njema"

Martino atakuwa na muda mchache wa kujiandaa kitu ambacho kitakuwa ni mtihani katika kazi yake ya ukocha – kuiongoza Barcelona kutetea taji lake la La Liga, kurejesha hadhi ya Nou Camp katika ligi ya klabu Bingwa (Baada ya kipigo cha mbwa mwizi  cha 0-7 toka kwa Bayern Munich) na kuwashinda mahasimu wao Real Madrid wanaoongozwa na Carlo Ancelotti.
Barcelona ina ratiba ya kucheza mchezo wa kirafiki na Bayern Munich Jumatano: Mechi hiyo ni sehemu ya makubaliano  ya uhamisho wa nyota wa kimataifa Thiago Alcantara kwenda mabingwa hao wa Bundesliga na Ulaya pia.
Pia inaeleweka kwamba Martino hatakuwepo benchi kwenye mechi hiyo ya kirafiki baina ya Barcelona na Bayern Munich, ingawa anaweza kuanza kwenye mechi ya kirafiki itakayopigwa kati ya Barca na Valarenga ya Norwei itakayochezwa Ijumaa.
Uamuzi wa Martino juu ya Fabregas

Kocha mpya huyo wa Barcelona atakuwa na wakati mgumu kufanya maamuzi kwamba amruhusu Cesc Fabregas kwenda Manchester United ama la.

Muhispania huyo amehusishwa na ofa mbili ambazo hazikufanikiwa za Manchester United kutaka kumnunua, ofa ya mwisho ilikuwa pauni milioni 30. Kufuatia hili inaaminiwa kwamba Barcelona imeachia maamuzi hayo kwa kocha mpya, ambaye kwa sasa amepatikana Martino.

Ingawa bado kuna sababu zitakazomfanya Moyes aendelee kufadhaika, Kuna sababu kuu mbili za msingi.

Ya kwanza ni: Martino anaamini sana kuchezesha viungo zaidi na atamfikiria kucheza na viungo wenzake wa Hispania kama Andres Iniesta na Xavi Hernandes, kupitia gazeti mojawapo la mwaka jana Martino alisikika akisema “Aina ya uchezaji wa Barcelona haitabadilika, lakini itakuwa ni vigumu sana kudumisha mchezo huo bila ya wachezaji mahiri kama Iniesta, Xavi na Cesc”.  Inaeleweka kwamba kocha huyo mpya wa Katalans atakuwa na shauku ya kuendeleza huduma ya Fabregas klabuni hapo.

Sababu ya pili ni kuondoka kwa kiungo mwingine wa kihispania – Thiago Alcantara. Nyota huyo naye Manchester United ilimtafuta sana lakini juhudi za Moyes hazikufanikiwa kiungo huyo alipofikia hatua ya kuitosa Manchester United na kutimkia Bayern Munich jambo lililomfanya Moyes kumgeukia Fabregas.

Inaonekana Fabregas atabakia Nou Camp, angalau kwa msimu huu, na Moyes atalazimika kuangaza macho kwengine kuboresha nafasi yake ya kiungo.

0 comments:

Chapisha Maoni