Mpira wa miguu haukubaki
kama ulivyokuwa mwanzo tangu Sir Alex Ferguson alipotangaza kustaafu kuwa
meneja wa Manchester United mwishoni mwa msimu uliopita.
Kilikuwa ni kipindi
kingine cha kufurahisha kwa mashabiki wa mpira wa miguu siku ya Jumapili wakati
waliposhuhudia Mashetani hao wekundu wakinyanyua taji linguine bila ya kocha
wao maarufu Ferguson. Hata hivyo, wale wote wanaomis uwepo wake msimu huu wa majira ya
joto, watakuwa na shauku kubwa kusikia kile ambacho mzee huyu maarafu katika
historia ya mpira wa miguu ameandika kuhusu upendo wake kwa Barclays Premier
League.
![]() |
| Enzi zake Manchester United - Kitendo cha kutangaza kustaafu ukocha kiliwashtua mashabiki wengi |
Akiongea kuhusu uzoefu
wake kwenye gemu, wakati akiongoza moja ya klabu kubwa za mpira wa miguu
duniani kwa takribani miaka 27, Mscotish huyo anazungumzia hali ya michezo
katika ulimwengu wa kisasa.
Haya ndiyo maneno
aliyoandika kuhusu Ligi ya Uingereza, endelea kusoma upate maneno yake kamili.
Mpira wa miguu umekuwa
maisha yangu na nimepata fursa ya kuwa na klabu bora sana Manchester United.
Mashabiki, wachezaji,
wafanyakazi wenzangu – wote wameshiriki kufanya kitu Fulani cha kukumbukwa.
Mataji tuliyoshinda, magoli bora toka kwa wachezaji, mechi za kuvutia
tulizocheza, na michezo yote tuliyopoteza vyote navikumbuka sasa – yote yanapaswa
kuwa kwenye kumbukumbu klabu iliyofanya kwenye Mpira wa miguu wa Uingereza.
![]() |
| Ferguson anakiri kwamba, Mpira wa miguu umekuwa sehemu ya maisha yake na amefurahia mafanikio yake |
Mambo mengi yamebadilika
katika michezo tangu nilipowasili toka Aberdeen Novemba 1986, ikiwa ni pamoja
na upenzi na kiwango cha uelewa. Kumekuwa na mabadiliko kutoka msimu mmoja hadi
mwingine. Lakini kuna mabadiliko kwa ujumla kwenye Ligi ya Uingereza
ukilinganisha na miaka 27 iliyopita.
Katika ligi mbalimbali,
viwanja vya michezo si kama ilivyokuwa zamani, maendeleo ya wachezaji hayakuwa
kama ilivyo sasa, waliokuwa wakirusha habari za michezo hawakuweza kurusha moja
kwa moja kwenye TV kama ilivyo sasa, mashabiki hawakuwa wakisikilizwa na
serikali zilikuwa zikipishana na michezo.
![]() |
| Alipoteuliwa: Sir Alex Ferguson amekiri kwamba Mchezo wa mpira una sura mpya kuliko alipowasili Old Trafford |
Manchester United, labda
zaidi ya klabu nyingine yoyote, imeleta chachu ya mabadiliko katika michezo
Uingereza katika muda wote wa Ligi ya Uingereza. Uwajibikaji wa klabu katika
kuwekeza katika kila Nyanja kunaiwezesha kung’ara.
Wachezaji wa kiwango cha
juu wote wamechangia kununua na kuendeleza mali za Old Trafford na Carrington
kwa wachezaji na mashabiki; Mipango ya kijamii inatuunganisha na jamii kwa
maendeleo ya sasa na baadaye – klabu imejiweka katika hali ambayo kila klabu
katika ligi ya Uingereza inapambana kuifikia, mara nyingine zinafanikiwa
kufika.
Changamoto
zinazojitokeza msimu baada ya msimu, zinatufanya tujitahidi kufanya vizuri
zaidi ya mwanzo. Katika kipindi changu wapinzani walipanda na kushuka. Wengine
wamebaki na wengine wanaendelea kupambana. Lakini upinzani ndiyo afya na ndicho
kinachoipa ligi hii ladha kuliko ligi nyingine za Ulaya.
Tunatambua kwamba hakuna
timu inayotaka kushindwa, Ubora wa Ligi ya Uingereza umekuwa ukiongezeka mwaka
kwa mwaka. Haikuwa kitu rahisi kutwaa ubingwa, kupata mchanganyiko mzuri wa
wachezaji – vijana wanatofautiana fikara.
![]() |
| Mfano Halisi: Ferguson ameshiriki kukuza vipaji, kama Cristano Ronaldo ambaye ni miongoni mwa wachezaji bora sasa |
Mataji, ya nyumbani na
yale ya Ulaya, ninachojivunia ni utamaduni wa vijana walioendeleza kutokana na
maono ya Matt Busby kwa klabu. Wachezaji
mahiri kama Ryan Giggs, Paul Scholes na Gary Neville walifanya klabu kuwa na
viwango vitakavyodumu daima.
Kumekuwa na wachezaji
wanaohitimu toka Manchester United Academy katika kila timu yangu ninayopanga. Vijana
wetu wa umri chini ya miaka 21 wameshinda kombe la Barclays chini ya umri wa
miaka 21 msimu huu kukiwa na wachezaji nane toka Old Trafford. Ari hii ya
kukuza vipaji toka nyumbani itazaa matunda siku moja.
![]() |
| Darasa la 92: Ferguson akiwa Manchester United ameendelea kukuza vipaji kupitia Academy yake. |
Kuna vijana wenye vipaji
katika nchi hii na kama wakipewa mafunzo sahihi, Ligi yote ya Uingereza
itafaidi matunda ya kazi hiyo njema inayofanywa na klabu.
Nimefurajia msimu wangu
wa mwisho, si kwasababu tumeshinda Ubingwa wa Uingereza kwa mara ya kumi na
tatu. Lakini haikuwa bahati kuutwaa ubingwa. Tulikuwa na haki: wachezaji wadogo
waliopata mafunzo, timu imara yenye viwango ambayo haikuwa tayari kushindwa –
tulikuwa nyuma kwa jumla ya point 29 msimu huu.
Umati wa watu mkubwa
sana. Niliagwa vizuri sana kwenye msimu wangu wa mwisho, lakini mechi yangu ya
mwisho katika Old Trafford ni jambo ambalo Mimi na familia yangu hatutasahau
kamwe.
Premier League ni ligi
inayotambulika kwa jinsi ilivyo maarufu na kuwa na mashabiki wengi.
Si Old Trafford tu– pia safari za Goodison, St. James’,
Anfield na White Hart Lane zilikuwa miongoni wa ziara zilizotoa ushirikiano. Ni
historia na utamaduni wa mchezo wa Uingereza vilivyoleta mafanikio. Nitakumbuka
haya yote daima. Lakini nitafurahia kutazama Barclays Premier League kuwa na
misimu mingine mizuri, yenye kuvutia na kutoa wachezaji wenye ubora.
![]() |
| Ferguson na Familia yake hawatosahau kamwe jinsi alivyoagwa siku ya mechi yake ya mwisho |













0 comments:
Chapisha Maoni