![]() |
| Kocha wa Arsenal iliyojichukulia point tatu za muhimu jana dhidi ya Marseille |
Arsene Wenger amedai Arsenal
haiogopi chochote katika Ligi ya Mabingwa Ulaya “Champions League” baada ya
kufanikiwa kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya Marseille katika kundi F.
Napoli nayo iko kileleni
mwa kundi F ikiwa imefungana point sawa na Arsenal na magoli pia baada ya
kuizika Borussia Dortmund 2-1 katika uwanja wa San Paolo.
Arsenal imepata ushindi
huo baada ya Theo Walcott kuifungia bao la kwanza na Aaron Ramsey kuweka bao la
pili kimiani.
Wenger alisema: ‘Mara zote tunajitahidi kushinda, na imekuwa hivyo.
'Tumecheza mechi nyingi
ugenini tukiwa katika hali ya changamoto ya kufungwa.
'Lakini jambo la
kufurahisha ni uwezo tulioonyesha, nilijua ni muhimu sana kutumia nafasi hii
kujinyakulia point tatu.
'Jana nilisema
tunahitaji point 10, nadhani point tatu sasa ni mwanzo mzuri.
'Nilidhani ungekuwa
mchezo mgumu kwasababu hata Marseille walikuwa wamejiandaa vema.
![]() |
| Theo Walcott akishangilia bao lake dhidi ya Marseille katika ushindi wa 2-1 |
![]() |
| Mesut Ozil alionyesha kiwango kizuri kwa mara nyingine tena |
'Marseille walianza vema
kipindi cha kwanza lakini hatukufanya makosa kwenye safu ya ulinzi.
'Nilihisi tusingefanya
chochote kwa jinsi nilivyoona mchezo kipindi cha kwanza, Marseille walikuwa
wakikimbiza sana na wakimiliki mpira muda mwingi. Walipoa kipindi cha pili na
tuliamua kuitumia nafasi hiyo vizuri.'
![]() |
| Aaron Ramsey alifanikiwa kufunga goli lake la sita la msimu huu na kuiwezesha Arsenal kupata bao la pili |
Ramsey, ambaye
alionyesha kiwango kikubwa alisema: 'Tuliwahi kucheza hapa tukashinda- Nimefunga pia, tumefanya kama ilivyo desturi
yetu na tumepata ushindi muhimu. Ni jambo la kujivunia.
'Nafurahia jinsi
ninavyocheza kwa sasa, Nacheza kwa kujiamini na kwa namna nzuri ya kuwakabili
mashabiki.







0 comments:
Chapisha Maoni