The reliable source of sport news

Jumatano, Julai 31, 2013

Arsenal inamhitaji Suarez au Song?

31.7.13 By Unknown No comments

Tangu uhamisho wa pauni milioni 15 kwenda Barcelona, Kipaji cha Song uwanjani kimekuwa hakitambuliki kwa walio wengi sasa.

Je, ni sawa Song kufikiria kurudi Arsenal tena?

Song, 25, amecheza michezo isiyopungua 38 kwa msimu akiwa Arsenal misimu minne iliyopita alipokuwa Arsenal na akatambulika kwa ustadi wa kazi yake nafasi ya kiungo na kwa upande mwingine kiungo mkabaji.
Alithaminiwa sana katika msimu wake wa mwisho Arsenal, ambapo alicheza mechi 46 akifunga goli moja na kutoa pasi 14 za magoli. 
Hakika anakumbukwa katika msimu huu kwa ushirikiano wake na Robin Van Persie uliowafanya mabeki wengi kushindwa kuizuia Arsenal.
Tangu aondoke umepita mwaka sasa, Song amepata fursa ya kuichezea Barcelona mara 20 tu, hajafunga goli hata moja na amefanikiwa kutoa pasi moja ya goli kwa miamba hao wa Catalan. 
Hajaweza kuwashawishi mashabiki wa Barcelona, ushawishi wake umekuwa mdogo sana. 
Ingawa Arsenal imekuwa klabu inayouza wachezaji miaka ya karibuni, lakini mwaka huu imeshindwa kufanya hivyo. 
Sasa wanahitaji kununua wachezaji wakubwa na Luis Suarez akiwa moto moto midomoni mwa mashabiki wa Arsenal na kwa nia njema Arsenal imepeleka ofa kadhaa kwa ajili ya nyota huyo raia wa Uruguay.
Lakini uchaguzi mrahisi kwa Arsenal utakuwa Alex Song. Mchezaji aliyethaminiwa na Arsenal na ameichezea michezo mingi lakini hapewi nafasi Barcelona. 

Kwa kiwango cha fedha walicho nacho Arsenal itakuwa rahisi kwao kuboresha kikosi chao kwa kumrejesha nyota huyo Arsenal.

MAONI YAKO NI YA MUHIMU SANA

0 comments:

Chapisha Maoni