The reliable source of sport news

Jumanne, Julai 30, 2013

David Moyes alikuwa akilala kwenye Gari - Soma hapa ujionee mwenyewe

30.7.13 By Unknown No comments

David Moyes, ambaye sasa ni Meneja wa Manchester United, akiri kwamba alilala kwenye gari wakati wa kombe la dunia lililofanyika Ufaransa mwaka 1998.
Kipindi hicho, wakati akianza kujifunza shughuli za umeneja wa mpira wa miguu, Moyes alianza kutafuta namna mbalimbali za kuvumbua wachezaji wenye vipaji sehemu tofauti tofauti duniani. Mscotish huyo amekiri kwamba mara nyingine ilimbidi alale kwenye gari wakati wa ziara yake hiyo. 

Akiongea na watangazaji, Moyes said: "Kipindi cha kombe la Dunia kule Ufaransa mwaka 1998, Ndiyo tu nilikuwa nimeteuliwa kuwa meneja wa Preston. Nilikiomba chama cha wataalamu wa mpira kuniwezesha kifedha iIi niende kwenye kombe la dunia kwa mafunzo.
"Niliziandikia nchi nyingi kuona kama nigepata fursa ya kwenda kutazama mafunzo.
"Aliyenijibu alikuwa Craig Brown wa Scotland – na mimi pia nilikuwa mscottish.
"Nilipata tiketi kutazama baadhi ya michezo, lakini hazikutosha. Lakini nilikodi gari dogo. Nilipewa fedha na PFA. Sikuwa nikipata fedha za kutosha.
"Mwishoni ilinilazimu kuendesha na ilinibidi kulala kwenye gari mara kadhaa. Hilo ndilo nililofanya kuongeza ujuzi zaidi."
Maisha ni tofauti sasa kwa bosi huyo wa Mashetani wekundu – Moyes amerudi toka ziarani ambako alizitembelea Japan, Thailand, Australia na Hong Kong. 
Na ndani ya kipindi cha wiki mbili, Agosti 11, kocha huyo mwenye umri wa miaka 50 atakuwa na kibarua cha kuiongoza timu yake uwanja wa Wembley dhidi ya Wigan Athletic mechi ya ngao ya Hisani.

Toka kulala kwenye gari hadi Old Trafford – imekuwa ni safari kwa David Moyes.

0 comments:

Chapisha Maoni