The reliable source of sport news

Alhamisi, Agosti 15, 2013

Real Madrid imetenga Euro milioni 110 pamoja na Fabio Coentrao ili kumnasa Gareth Bale

15.8.13 By Unknown No comments

Ukurasa wa mbele wa gazeti la Madrid, AS kwa mara nyingine limeandika habari za Gareth Bale leo Alhamisi kuwa kuna maendeleo yaliyofanyika katika mchakato wa uhamisho wa nyota wa Tottenham Hotspur, Gareth Bale.
Kwa mujibu wa Marco Ruiz, mwanahabari aliyekuwa akimfuatilia Gareth Bale akiwa kwenye timu ya Taifa ya Wales, amedai kuwa mwenyekiti wa Tottenham Daniel Levy yuko karibu kuikubali ofa ya Euro milioni 110 pamoja na beki wa kushoto wa Real Madrid Fabio Coentrao.
Spurs awali ilikuwa akimuhitaji Jese Rodriguez au Alvaro Morata kujumuishwa kwenye dili hilo pamoja na fedha, lakini Real Madrid itamtoa Coentrao wanayempa thamani ya Euro milioni 30.
Levy anahitaji Euro milioni 90 pamoja na Coentrao, Real Madrid inaamini kuwa Euro milioni 85 pamoja na mchezaji huyo wa zamani wa Benfica inatosha.
Tottenham wanaonekana kutokuwa na haraka kukamilisha mchakato huo, wakati Real Madrid inajitahidi kukamilisha swala hili mapema iwezekanavyo kabla msimu haujaanza.
“Chanzo kimoja” kimenukuliwa na AS: ”Bale ameshikilia msimamo wake kwa wiki tatu sasa. Hataki kufanya mazoezi wala kucheza mechi yoyote… inaonekana amedhamiria kweli.”
Mwishoni, AS linaongeza kuwa Spurs haijakata tama kumshikilia Bale na bado wanafikiria kufanya mazungumzo kwa ajili ya mkataba mwingine na raia huyo wa Wale siku za usoni.

Kava ya mbele ya gazeti la AS hii hapa.



0 comments:

Chapisha Maoni