![]() |
| Nje Ulaya: Michael Essien (kushoto) amekuwa akiishia kusugua benchi mechi tatu za Chelsea mwanzoni mwa msimu na ametemwa kikosi cha Ulaya |
Essien alikuwa kwa mkopo Real Madrid
msimu uliopita na amerejea Stamford Bridge chini ya kocha Jose
Mourinho.
Lakini mchezaji huyo mwenye umri wa
miaka 30 amekuwa akiishia kusugua benchi katika mechi zote tatu kati ya
nne za ufunguzi za The Blues msimu huu na hatacheza michuano ya Ulaya.
Nahodha wa Scotland, Fletcher amecheza
mechi 13 tu tangu alazimike kusimama soka kwa maradhi mwaka 2011.
Uamuzi wa David Moyes kumtema Fletcher
katika kikosi cha United unatokana na kuhofia mchezaji huyo mwenye umri
wa miaka 29 hataweza kurejea kwenye kikosi cha kwanza mwaka huu na
wakati hatua ya makundi ya Ligi Mabingwa inamalizika Desemba.
Agosti, Fletcher alijizuia kufika kwenye
Uwanja wa mazoezi wa United, AON Complex mjini Carrington.

Nje: Darren Fletcher hajacheza soka
tangu Desemba
"Bado niko mbali na viwanja vya mazoezi
hadi sasa, tu kwa sababu ni vigumu kwenda huko wakati hufanyi mazoezi.
Nimezungumza na kocha, anaonekana
poa na tumejadili mipango ya mbele,"alisema mchezaji huyo ambaye
ameongeza akiwa fiti ataanza mazoezi mara moja.

Bado yuko mbali: Fletcher amesema haendi
Carrington kwa sababu hafanyi mazoezi

Wa mkopo: Adnan Januzaj hayuko kwenye
orodha ya wachezaji 25 wa Man United wa Ulaya
Wakati huo huo, kinda mwenye kipaji,
Adnan Januzaj, ambaye alikwenda kwenye ziara ya klabu ya kujiandaa na
msimu Mashariki ya Mbali na Australia na kufanya vizuri pia ametemwa
kwenye kikosi hicho.
Inafahamika Mbelgiji, ambaye atapewa
Mkataba mpya wa miaka mitano katika klabu hiyo, anaweza kutolewa kwa
mkopo.
Pamoja na hayo, makinda wenzake Sam
Johnstone, Jesse Lingard, Tom Thorpe, Will Keane na Larnell Cole
wameorodheshwa katika kikosi cha pili, Man United B.
Wachezaji wapya Wilfried Zaha na
Marouane Fellaini wamo kwenye kikosi hicho.
VIKOSI VYA TIMU ZA UINGEREZA KATIKA MICHUANO YA LIGI YA MABINGWA ULAYA MSIMU HUU NI HIVI...
Arsenal: Szczęsny,
Sagna, Mertesacker, Vermaelen, Koscielny, Rosický, Arteta, Podolski,
Wilshere, Özil, Giroud, Viviano, Walcott, Oxlade-Chamberlain, Ramsey,
Monreal, Cazorla, Flamini, Fabiański, Sanogo, Jenkinson, Gibbs, Ryo,
Bendtner. Zelalem
Chelsea: Cech,
Schwarzer, Ivanovic, Cole, Luiz, Cahill, Terry, Azpilicueta, Bertrand,
Ramires, Lampard, Oscar, Mikel, De Bruyne, van Ginkel, Hazard, Willian,
Torres, Mata, Schurrle, Ba, Eto'o
Manchester City: Hart, Pantilimon, Johansen, Richards, Kompany, Zabaleta, Lescott, Kolarov, Clichy, Demichelis, Nastasic, Boyata, Milner, Nasri, Garcia, Navas, Rodwell, Silva, Fernandinho, Toure, Negredo, Dzeko, Aguero, Jovetic
Manchester United: De Gea, Lindegaard, Rafael, Evra, Jones, Ferdinand, Evans, Smalling, Vidic, Fabio, Buttner, Anderson, Giggs, Carrick, Nani, Young, Cleverley, Valencia, Kagawa, Zaha, Fellaini, Rooney, Hernandez, Welbeck, van Persie
Celtic: Forster, Zaluska, Izaguirre, Ambrose, van Dijk, Wilson, Mulgrew, Mouyokolo, Lustig, Biton, Brown, Commons, Ledley, Rogic, Samaras, Stokes, Boerrigter, Balde, Pukki
Manchester City: Hart, Pantilimon, Johansen, Richards, Kompany, Zabaleta, Lescott, Kolarov, Clichy, Demichelis, Nastasic, Boyata, Milner, Nasri, Garcia, Navas, Rodwell, Silva, Fernandinho, Toure, Negredo, Dzeko, Aguero, Jovetic
Manchester United: De Gea, Lindegaard, Rafael, Evra, Jones, Ferdinand, Evans, Smalling, Vidic, Fabio, Buttner, Anderson, Giggs, Carrick, Nani, Young, Cleverley, Valencia, Kagawa, Zaha, Fellaini, Rooney, Hernandez, Welbeck, van Persie
Celtic: Forster, Zaluska, Izaguirre, Ambrose, van Dijk, Wilson, Mulgrew, Mouyokolo, Lustig, Biton, Brown, Commons, Ledley, Rogic, Samaras, Stokes, Boerrigter, Balde, Pukki
*Zingatia;
vikosi vyote vimeambatanishwa na vikosi vya timu B, vinavyohusisha
wachezaji wa umri usiozidi miaka 21




0 comments:
Chapisha Maoni