The reliable source of sport news

Alhamisi, Septemba 05, 2013

WAYNE ROONEY AMEPOST FACEBOOK PICHA INAYOONYESHA JINSI ALIVYOJERUHIWA KICHWANI

5.9.13 By Unknown No comments

Picha ya Wayne Rooney ikionyesha jinsi alivyoumia kichwani
Straika wa Uingereza, Wayne Rooney amepost picha mtandaoni picha inayoonyesha jinsi alivyojeruhiwa kichwani, majeraha yaliyomfanya akose mechi za kuwania kufuzu kombe la Dunia.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27, alikosa mechi ya Manchester United wakati ilipocheza dhidi ya Liverpool (Waliyokula kichapo cha 1-0) Jumapili iliyopita baada ya David Moyes kuthibitisha kuwa amepata majeraha kichwani kufuatia kugongana kwa bahati mbaya na mchezaji mwenzake Phil Jones walipokuwa kwenye mazoezi.
Moyes alieleza kuwa ana imani Rooney atapona mapema na kujiunga na wenzake kwenye timu ya Taifa itakayocheza dhidi ya Moldova na Ukraine.
Rooney ameweka picha inayoonyesha majeraha yake kwenye ukurasa wake wa facebook Jumatano jioni ikifuatiwa na maelezo machache kama yanavyoonekana kwenye ayah ii hapa chini.
"Baadhi ya watu wanajiuliza kama nitaitumikia Uingereza kipindi hiki ama la, ki ukweli nimeamua kujito kwenye michezo miwili ya kuwania kufuzu kombe la Dunia," aliandika.
Ukurasa wa Facebook wa Wayne Rooney ukionyesha jinsi alivyoandika kuhusu majeraha yake ya kichwani
"Hakuna shaka, napenda kuwa pamoja na wenzangu kuwania kufuzu kucheza kombe la Dunia. Nina imani watu wakiona picha hii wataelewa ni kwanini siwezi kucheza kipindi hiki."
Mchezaji mwenzake Theo Walcott alieleza jana kuhusu kidonda hicho "kinafanana na majeraha ya kwenye filamu za kutisha".
Uingereza itaumana na Moldova na Ukraine, kwa sasa iko nyuma ya vinara Montenegro kwa point 2 lakini ikiwa na mchezo mmoja mkononi.
Rooney, ambaye alihusishwa sana na uhamisho kwenda Chelsea kabla dirisha la usajili halijafungwa, aliamua kubaki Manchester United.
Lakini majeraha hayo yanamaanisha Rooney, aliyeichezea England mara 84 na kufunga magoli 36, atakosa mechi kadhaa za kuwania kufuzu kombe la dunia wakati wachezaji wenzake Danny Welbeck, na nyota wa Liverpool Daniel Sturridge watakaposhuka dimbani.


0 comments:

Chapisha Maoni